Tuesday, October 24, 2017

RAIS WA TFF "AMUUMA SIKIO" KOCHA WA TIMU YA TAIFA YA WANAWAKE YA SWEDEN



Kocha Mkuu wa timu ya soka ya taifa ya Sweden, Mariane Sundhage  Oktoba 23, 2017 amekutana na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dk. Kebwe Stephen Kebwe katika Ofisi ya Mkoa na kufanya mazungumzo yenye lengo la kuboresha soka la wanawake nchini.

Kadhalika, Kocha Mariane Sundhage amefanya mazungumzo yanayofanana na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF), Wallace Karia ambaye baadaye aliongozana naye kwenda kuangalia Kliniki kwenye Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Bigwa.


Katika Kliniki hiyo, mbali ya Rais Karia wengine waliokuwako kushuhudia kliniki hiyo ni Mwenyekiti wa Chama cha Soka la Wanawake (TWFA), Amina Karuma na Mjumbe wa Kamati ya Maendeleo ya soka la Wanawake, Mia Mjengwa.

Kocha Mariane Sundhage yuko nchini Tanzania na kesho Jumanne Oktoba 24, 2017 anatarajiwa kuwa na kliniki maalumu kwenye Uwanja wa Karume, Ilala jijini Dar es Salaam.
Kocha huyo mahiri ambaye mbali ya Sweden ambako anafundisha sasa, tayari alikwisha kuzinoa timu za taifa za  Marekani na China.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Ufundi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Salum Madadi, kliniki hiyo itaanza saa 3.30 asubuhi mpaka saa 6.00 mchana baada ya hapo kocha huyo atakuwa na nafasi ya kuzungumza na wanahabari.


“Karibu sana wanahabari kesho kushuhudia ufundi wa Kocha Pia Sundhage akizinoa baadhi ya timu ambazo TFF imezialika wakiwamo wachezaji wa timu ya taifa,” amesema Madadi alipokuwa anatambulisha ziara ya kocha huyo.

No comments:

Post a Comment