Tuesday, June 18, 2019

Breaking News:Lori Lagonga treni Dodoma....Wajeruhiwa 29


Watu 29 wamejeruhiwa baada ya lori kugonga treni jijini Dodoma. Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Protas Katambi amesema leo asubuhi Jumanne Juni 18, 2019 kuwa ajali hiyo imetokea jana saa 5.30 usiku.

Amesema ametoa maagizo kwa vyombo vya usalama kumsaka dereva wa lori ambaye inasemekana aliruka kutoka kwenye lori baada ya ajali hiyo kisha kutokomea kusikojulikana.

Shughuli ya kuondoa mabehewa ya treni inaendelea huku ulinzi ukiwa umeimarishwa katika eneo la tukio huku polisi waliokuwa na silaha wakiwa wameimarisha ulinzi katika tukio.

No comments:

Post a Comment