Wednesday, March 7, 2018

Majambazi wamvamia na kujaribu kumkata miguu mwanariadha wa Afrika Kusini kwa msumeno

Mhlengi Gwala

Mwanariadha nchini Afrika Kusini nusura akatwe miguu kabisa aliposhambuliwa na kundi la wanaume alipokuwa anafanya mazoezi Jumanne alfajiri.

Polisi wanasema mwanaraidha huyo hakuwafahamu wanaume waliomshambulia lakini inavyoonekana ni kwamba shambulio hilo sio la wizi wa kawaida, na kwa hivyo maafisa wanachunguza uwezekano wa njama nyingine.
Mwanariadha Mhlengi Gwala mwenye umri wa miaka 26 anapokea matibabu katika hospitali moja huko KwaZulu-Natal baada ya kushambuliwa na wanaume watatu katika mji wa pwani Durban.
Haijulikani dhamira ya shambulio hilo lakini polisi wanasema mwanariadha Gwala aliwapa washambuliaji simu na pesa alizokuwa nazo, ambao badala yake walimsukuma chini na kumburura katika kichaka kilichokuwa karibu na kujaribu kumkata miguu yake kwa kutumia msumeno usiokuwa na makali.
Msemaji wa polisi Nqobile Gwala ameiambia BBC kwamba uchunguzi umeanzishwa wa jaribio la mauaji.
Amekitaja kisa hicho kama cha "kushutusha na chenye kuvunja moyo".
Mkasa huo umewatia wasiwasi raia wengi nchini Afrika kusini - hata iwapo ni nchi inayoshuhudia visa vingi vya uhalifu.
Marafiki zake Gwala , wanaowasiliana na madakatari wanaomtibu, wanasema atapona kikamilifu lakini taratibu.
Hata hivyo atahitaji kufanyiwa upasuaji.
Wengi wanatumia mitandao ya kijamii kushinikiza kukamtwa kwa wahalifu hao na wapewe hukumu nzito gerezani.

No comments:

Post a Comment