Wednesday, January 17, 2018

Japan yaonya kuhusu urafiki ambao umeonekana kutoka Korea Kaskazini

Kim Jong-un


Japan imeuambia mkutano wa kimataifa kuhusu Korea Kaskazini kuwa dunia isifumbwe macho na urafiki amabo umeanza kuonekana kutoka kwa Korea Kaskazini.

Matamshi ya waziri wa mashauri ya nchi za kigeni Taro Kono huko Canada, yanakuja huku Korea Kaskazini na Kusini wakijadili mipango ya Korea Kaskzini kushiriki mashindano ya msimu wa baridi nchini Korea Kusini.
Mawaziri 20 wa mashauri ya nchi za kigeni huko Vancouver walikubaliana kuongeza shinikizo didi ya Korea Kaskazini.
Lakini waliunga mkono mazungumzo yanayoendelea kati ya Korea Kaskazini na Kusini.
Kwa miaka miwili iliyopita Korea Kaskazini kwa haraka iliboresha programu yake ya makombora licha ya kuwepo vikwazo vya kimataifa.
Jaribio la mwisho la kombora la masafa marefu la tarehe 28 Novemba lilizua awamu mpya ya vikwazo kutoka kwa Umoja wa Mataifa ambavyo vililenga uagizaji wa mafuta na usafiri.
Lakini kiongozi wa Korea Kim Jong-un mapema Januari alisema kuwa yuko tayari kwa mazungumzo na Korea Kusini na kupendekeza kutuma timu kwa mashindano huko Pyeongchang mwezi ujao.

No comments:

Post a Comment