Friday, February 9, 2018

BALOZI WA NABII MKUU TANZANI MTUME SEKELA N'TONDOLO JANA AMEONGOZA IBADA YA CHUO CHA MANABII.

 PICHANI JUU NI BALOZI WA NABII MKUU TANZANIA MTUME SEKELA N'TONDOLO

Imeelezwa kuwa wakristo wengi wamekuwa wakiishi kwa hofu kwa sababu hawataki kumshirikisha mungu shida zao.

 hayo ni moja ya mahubiri aliyokuwa akifundisha balozi wa nabii mkuu mtume Sekela N'tondolo siku ya jana tarehe 08/02/2018 katika ibada ya chuo cha manabii iliyofanyika hemani kisongo arusha.

akifundisha somo ;enye kichwa kisemacho kubadilishwa katika uwepo wa mungu amesema kuwa watu wanatakiwa wautambue uwepo wa mungu uliopo ndani yao kwani wasipotambua wanamfanya mungu anyamaze badala ya kuwajibu mahitaji yao

ibada ya chuo cha manabii ndani ya HUDUMA YA NGURUMO YA UPAKO  huwa ni kila siku za jumanne na alhamisi,na watu mbalimbali hupata nafasi ya kuhudumiwa kwa karibu zaidi na watumishi wa mungu wanaotumika chini ya mkono wa kinabii.


No comments:

Post a Comment