Wednesday, September 13, 2017

Mwanasheria Mkuu wa serikali amzungumzia Lissu


Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju amefunguka kuhusu sakata la Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu kupigwa risasi na watu wasiojulikana na kusema kuwa kwa sasa jambo hilo waachiwe polisi na vyombo vya usalama.

Akiongea leo bungeni George Masaju alianza kwanza kwa kutoa pole kwa Mbunge Tundu Lissu kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana na kusema serikali inalaani vikali kitendo hicho alichofanyiwa Tundu Lissu.

"Naomba kutoa pole kwa Tundu Lissu kwa majeraha aliyopata kutokana na kupigwa risasi na watu wasiojulikana sisi kama serikali tunalaani vikali jambo hili, kwa kuwa sasa jambo hili lipo kwa jeshi la polisi, tuviachie vyombo vya usalama naamini watafanya upelelezi kwa haraka" alisema George Masaju

Mbunge Tundu Lissu kwa sasa yupo nchini Kenya akipatiwa matibabu kufuatia kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 mjini Dodoma.

No comments:

Post a Comment