Wednesday, September 13, 2017

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI GERSON LWENGE

Waziri wa Maji na umwagiliaji Mhandisi Gerson Lwenge amesema Serikali inatekeleza ujenzi wa mradi wa bomba la maji safi kutoka ziwa viktoria kuelekea katika mji wa Ngudu na vijiji vinavyopitiwa na mradi huo  ili kuwapunguzia wananchi adha ya maji wanayoipata.


Waziri Gerson Lwenge amesema hayo bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la Machimba Mashauri Ndaki mbunge wa Maswa Magharibi aliyetaka kujua
ni lini serikali itakamilisha ujenzi wa mradi wa bomba la maji kutoka Ziwa Viktoria.
Amesema kuwa serikali kupitia mpango wa sekta ya maji imetekeleza mradi wa maji katika maeneo ya malampaka, Sayusayu, Masayi, Njia panda na Senga mwarugesha ambayo maeneo hayo wananchi  hupata maji huku akiongeza kuwa miradi ya maji ya lalago, Mandhang’ombe na Jija ikiwa inaendelea kujengwa ambapo ujenzi wake umefikia asilimia 65.
Aidha amesema kuwa Serikali imekamilisha usanifu na makabrasha ya Zabuni kwa miradi ya maji ya Mwabulimbu, mwamanenge na Badi ambao utahudumia vjiji vitatu vya Muhiba, Jibu na Badi huku akisema kuwa miradi hiyo itafanyika katika awamu ya pili ya program ya maendeleo sekta ya maji. 



No comments:

Post a Comment