Thursday, September 7, 2017

Zungu: Mgodi wa almasi ni sawa na shamba la bibi

Mwenyekiti wa kamati ya Spika iliyochunguza uchimbaji wa almasi, Azzan Mussa Zungu amesema vita ya kupigania rasilimali za nchini imewaunganisha wabunge wa vyama vyote.


Kamati hiyo iliyoundwa na Spika wa Bunge, Job Ndugai ilipewa jukumu la kutathmini mfumo wa uchimbaji, usimamizi, umiliki na udhibiti wa madini ya almasi nchini.

Zungu ambaye ni mbunge wa Ilala, amesema leo Septemba 7 kuwa wabunge wote wanatamani rasilimali za Tanzania zitumike na Watanzania na si kuwapa furaha wawekezaji kutoka nje.

“Kamati ilipoenda Shinyanga ilibaini upungufu mkubwa katika usimamizi wa madini yanayochimbwa na hata wachimbaji wanapofanya ndivyo sivyo, bodi ya almasi haichukui hatua yoyote,” amesema Zungu.

Amesema bodi ya almasi imewaangusha Watanzania kwa kushindwa kusimamia vizuri madini hayo ya vito kama ambavyo imepewa dhamana.

“Mgodi wa almasi uliopo Shinyanga umekuwa kama shamba la bibi, viongozi wa Serikali walikuwa wanaenda kule kuchota fedha na kugawana,” amesema.

Amesema hayo wakati wa kukabidhi ripoti kwa Rais John Magufuli, Ikulu jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment