Thursday, August 17, 2017

MAPOROMOKO YASITISHA MAISHA YA WENGI NCHINI SIERRA LEONE.

Zaidi ya watu 500 wametoweka kufuatia maporomoko ya matope na mafuriko kwa mujibu wa msemaji wa Rais maporomoko hayo yamesababisha uharibifu mkubwa katika maeneo kadhaa ya mji mkuu wa Free town nchini Sierra Leone.
Responsive image
Mapema Rais Ernest Bai Koroma aliomba usaidizi wa dharura  kwa kusema kwamba  jamii nzima ilikuwa imeangamia.
Siku ya Jumatatu takriban watu 400 wamethibitishwa kufariki baada ya maporomoko ya matope katika eneo la Regent na mafuriko katika maeneo mengine mjini Freertown .
Shirika la msalaba mwekundu limeonya kuwa hakuna muda wa kutosha kuweza kuwaokoa manusura.  Mazishi ya pamoja ya waathiriwa yanatarajiwa kufanyika siku ya Jumatano ili kupunguza idadi ya wafu katika chumba cha kuhifadhia maiti.
Msemaji wa Rais Abdulai Baraytay aliambia BBC kwamba miili ilikuwa ikitolewa katika matope hayo na vifusi.
Umoja wa Mataifa umesema kuwa kwamba wafanyakazi wake nchini Sierra Leone wamekuwa wakisaidia katika juhudi za kuwaokoa manusura.
Chanzo BBC Swahili.

No comments:

Post a Comment