Tuesday, August 1, 2017

WATU MBALIMBALI WAMEKARIBISHWA LEO JUMANNE KATIKA IBADA YA CHUO CHA MANABII .



Kadinali wa pili wa huduma ya Ngurumo Ya Upako Mchungaji Elizabeth Humprey amewaalika watu kutoka sehemu mbalimbali kuhudhuria ibada ya
katikati ya wiki inayofanyika hii leo katika hema la kukutania kisongo Arusha.
Akizungumza na N.Y.U Radio amesema kuwa katika ibada ya katikati ya wiki watumishi wa mungu hufundisha neno la mungu kwa kifupi na mara baada ya neno la mungu hupita katikati ya watu kwa ajili ya kuwafungua watu kulingana na mahitaji yao.
Ameongeza kuwa ibada ya leo itakuwa ni ya baraka, hivyo watu watapokea miujiza, maongezeko na hatua mpya katika kila eneo.
Aidha amesema kuwa huduma ya ngurumo ya upako ipo kwa ajili ya watu wote kwani haichagui dini, kabila hivyo nguvu ya mungu ipo kwa ajili ya kuwahudumia watu wote.

 

No comments:

Post a Comment