Wednesday, July 19, 2017

ANTONIO CONTE: MENEJA WA CHELSEA ASAINI KANDARASI MPYA YA MIAKA 2.

Meneja wa Mabingwa wa England Chelsea, Antonio Conte, amesaini Mkataba Mpya ulioboreshwa wa Miaka Miwili.
Dili hii haiongezi muda wake wa Mkataba wa Miaka Mitatu aliosaini Mwaka 2016 bali imempa maslahi bora zaidi.
 
Meneja huyo kutoka Italy mwenye Miaka 47 amesema amefurahishwa mno na Mkataba huu Mpya na kuahidi kufanya bidii zaidi kupita Mwaka wake wa
kwanza uliozaa Ubingwa wa EPL, LIGI KUU ENGLAND.
Wakielekea kutwaa Ubingwa, Kikosi cha Conte kilishinda Jumla ya Mechi 30 zikiwemo 13 mfululizo ambayo ni Rekodi kwa Chelsea.
Mbali ya Ubingwa huo, Conte pia aliiongoza Chelsea kufika Fainali ya FA CUP waliyofungwa na Arsenal.
Ujio wa Conte huko Stamford, ulimwezesha Kocha huyo wa zamani wa Juventus na Timu ya Taifa ya Italy kuigeuza Chelsea iliyomaliza Nafasi ya 10 kwenye EPL Msimu wa kabla yake na kutwaa Ubingwa kwa kishindo.
Wachambuzi wanahisi mafanikio hayo yaliletwa na uamuzi wa Conte wa kugeuza mtindo wao wa Mazoezi na pia Mfumo wa Uchezaji wa kutumia Mabeki Watatu katika Fomesheni ya 3-4-3.

Chelsea – Mechi kuelekea Msimu Mpya:
22 Julai v Arsenal, Bird’s Nest Stadium, Beijing
25 Julai v Bayern Munich, National Stadium, Singapore (International Champions Cup)
29 Julai v Inter Milan, National Stadium, Singapore (International Champions Cup)
6 Agosti v Arsenal, Wembley Stadium (Community Shield)

No comments:

Post a Comment