Tuesday, July 18, 2017

ARSENE WENGER:NITATUMIA CHIPUKIZI UEFA EUROPA LIGI!

EUROPALIGI NICE 2

ARSENE WENGER ameripotiwa kuwa atawatumia Chipukizi wake kwenye Mashindano ya UEFA EUROPA LIGI ili Kikosi cha Kwanza cha Arsenal kitilie mkazo mbio za Ubingwa za EPL, LIGI KUU ENGLAND.
Wenger, ambae ameongezewa Mkataba wa Miaka Miwili wa kuwa Meneja wa Arsenal, yuko kwenye presha kubwa ya kuhakikisha Klabu hiyo inafanikiwa kwenye Msimu Mpya wa 2017/18. 
Msimu uliopita Arsenal ilimaliza Nafasi ya 5 kwenye EPL na hivyo kukosa kucheza UEFA CHAMPIONZ LIGI kwa mara ya kwanza katika Miaka 20.
Pia Arsenal hawajatwaa Ubingwa wa England tangu 2004.
Kwa mujibu wa duru za ndani ya Arsenal, Wenger hatawatumia Mastaa wake wakubwa kama  vile Alexis Sanchez, Alexandre Lacazette na Mesut Ozil kwenye UEFA EUROPA LIGI ili wakaze kwenye EPL.
Kwenye UEFA EUROPA LIGI Arsenal itaanzia Hatua ya Makundi na Droo ya kupanga Makundi hayo itafanyika Agosti 25.

No comments:

Post a Comment