Sunday, July 30, 2017

NABII MKUU MH DK GEORDAVIE AENDELEA KUWAHIMIZA WATU KUWA NA UPENDO MIONGONI MWAO.

Nabii mkuu Mh. Dk GeorDavie amewataka watu kuwa na upendo na mshikamano miongoni mwao ikiwa ni pamoja na kurekebishana wanapokosea na siyo kukandamizana.
 
Ameyasema hayo leo wakati akiongoza ibada ya jiji katika hema la kukutania chuo kikuu cha manabii kisongo ambapo maelfu ya watu kutoka sehemu
mbalimbali wamehudhuria ibada hiyo ya unabii mkuu.
Katika ibada hiyo Nabii Mkuu amefundisha na kutamka matamko mbalimbali ambayo yalikuwa baraka kwa wale waliohudhuria ibada hiyo.
Aidha amewataka watumishi wa Mungu kufanya kazi ya Mungu kwa bidii bila kukubali kuyumbishwa na kitu chochote katika utendaji kazi wao kwa ajili ya kuijenga serikali ya ufalme wa Mungu.
Pia Nabii Mkuu Mh Dk. GeorDavie ametangaza kuwa siku ya tarehe 9/9 mwaka huu anatarajia kufanya kongamano ambalo litakuwa la Tisa tangu kuanzishwa kwa makongamano katikahuduma ya  Ngurumo Ya Upako.
Pia katika ibada hiyo Nabii mkuu Mh Dk GeorDavie ametangaza jumapili ya tarehe 13 mwezi wa nane kuwa siku ya Pipa Day ambapo itafanyika Mjini Mwa Daudi Katika Bonde La Utulivu.
Wakati huo huo Nabii Mkuu Mh. Dk GeorDavie ametangaza kuwepo radioni siku ya kesho  katika kipindi cha kusapoti magurudumu ya Radio kuanzia majira ya saa mbili na nusu za usiku.

No comments:

Post a Comment