Tuesday, July 18, 2017

TRUMP AIONYA VENEZUELA.


Rais wa Marekani Donald Trump amesema Venezuela itakabiliwa na hatua za kiuchumi iwapo itaendelea na mipango yake ya kutaka kuandika upya katiba ya nchi hiyo.

Kufuatia onyo hilo alilolitoa, Rais Trump pia ameupongeza upinzani nchini humo kutokana na kupigania kwake demokrasia na kumuelezea Rais Nicolas Maduro kama kiongozi mbaya ambaye anaota ndoto za kuwa dikteta.
Upinzani nchini Venezuela umetoa wito wa kufanyika mgomo wa siku moja nchi nzima siku ya Alhamisi kama sehemu ya kampeni zake kupinga uamuzi huo wa Rais Maduro kubadili katiba.
Siku ya Jumapili mamilioni ya Wavenezuela walijitokeza kupiga kura ya maoni isiyo rasmi kupinga pendekezo hilo, lakini hata hivyo serikali ya nchi hiyo, ikasema zoezi hilo la upigaji kura si halali.

No comments:

Post a Comment