Monday, July 10, 2017

MCHUNGAJI KIONGOZI WA N.Y.U DUNIANI MAMA ANNA DAVIE ATANGAZA UJIO WA NABII MKUU SIKU YA JUMAPILI TAR 16.07.2017



Mchungaji kiongozi wa huduma ya ngurumo ya upako duniani mama Anna Davie ametangaza ujio wa Nabii Mkuu Mh Dk Geor Davie jumapili ijayo katika ibada ya jiji  hemani kisongo.


 mama anna davie amesema hayo jana katika ibada ya jiji  kwenye hema kla kukutania kisongo arusha tanzania ambapo pia mama alisema kuwa nabii atakuwepo hivyo ni vyema watu wakaja kwa wingi kuja kupokea jambo jipya maishani.
katika ibada hiyo ya jiji balozi wa nabii mkuu tanzania mtume Sekela Ntondolo  alitoa maagizo kwa niaba ya nabii mkuu ,amabapo maagizo hayo ni kwajili ya kuwawezesha watu kupata upenyo na hatua mpya katika maisha yao.
katika ibada hiyo nabii william james wa huduma ya ngurumo ya upako  tawi la Dar es Salaam  la city centre alifundisha somo lenye kichwa kisemacho nyumbani ambapo amewataka watu kupokea maonyo wakiwa nyumbani kwani ndiyo sehemu ya kwanza ya kupata malezi yatakayowasaidia maishani.
watu walihudhuria ibada hiyo pia wamefurahishwa na ibada hiyo ,ila pia juu ya ujio wa nabii mkuu tz jumapili ijayo na hivyo wamewataka watu waweze kuhudhuria ibada hiyo bila kukosa wakiwa na sadaka maalumju.



No comments:

Post a Comment